OTHER WEBSITE LISTS


Monday, September 12, 2011


wanusura wa ajali wakiwa wamekaa juu ya boya ili kuokoa nafsi zao wakati, chini ni maiti za watoto zikiwa zimelazwa chini baada ya ajali ya meli ya Mv spice islanders iliyotokea usiku wa kuamikia Jumamosi ya tarehe 10 September. ajali hii inapaswa kuangaliwa kwa undani zaidi kwani mbali na sababu kadha wa kadha ambazo watu wamesema kwamba ndio chanzo. kikubwa ni kujua kwamba shetani yuko kazini na jambo kubw analolifanya ni kuhakikisha anawapata watu wengi. watu wa Mungu ni kazi kwetu kuhakikisha kwamba tunabomoa kikakati ya shetani yote dhidi wa watu. na ni kwa njia ya maombi pekee ndio inaweza kusimamisha ajali za namna zote yani majini na nchi kazi ambazo zimekuwa zikijitokeza kila kukicha.

Saturday, September 10, 2011

SUALA ZIMA LA KIFO

SUALA LA KIFO

Nimekuwa nikifuatilia kwa makini kuhusu sUala la kufa, na haya ndiyo nikajifunza katika kufuatilia kwangu. La kwanza kabisa ni jinsi sUala hili lisivyotakiwa kuzungumzwa kufuatana na utamaduni na maadili ya kikwetu wa-Tanzania kama siyo Afrika. Kwenye nchi mojawapo jirani, mtu mmoja ambaye aliwahi hata kuwa waziri katika serikali ya nchi hiyo na ni mtu mwenye uwezo, alijiamulia kwamba badala ya kungoja akifa huku nyuma watu waamue wanamzikaje, yeye aliamua kutengeneza kwa kuchimba kaburi lake vizuri na kuta za ndani akazipamba kwa vioo. Kisha akajitengenezea jeneza zuri la kioo na ndani yake akaweka sanda nzuri, suti, viatu, shati na tai, vyote vya gharama kubwa toka nje ya nchi, kisha kuliweka hilo jeneza ndani ya hilo kaburi na kuegesha mfuniko mzuri wa nakshi juu ya hilo kaburi lakini likiwa ndani ya nyumba ndogo na nyumba hiyo iko ndani ya ua wake. Jambo lililotokea, wana kijiji walipata habari ya tukio hilo. Kwa bahati mbaya sana kukatokea wazungu wanasema “coincidence.” Mvua nayo ikakataa kunyesha sehemu hiyo wakati wa vipindi vyake kwa miaka kadhaa kuanzia kaburi hilo lilipochimbwa. Wanakijiji wakaunganisha kutokunyesha kwa mvua na hilo kaburi. Walichokifanya, walimwendea mheshimiwa huyo ambaye kwa miaka mingi kabla kustaafu toka kwenye siasa, alikuwa mbunge wao akipita pasipo kupingwa katika kila uchaguzi hadi hapo alipostaafu (sasa mheshimiwa huyo umri umekwenda ingawa anaonekana bado kwenye shughuli mbalimbali). Wanakijiji walimlazimisha kuvunja jeneza lake na kaharibu kabisa kaburi. Hivi navyoandika, hakuna kaburi wala jeneza lililotayarishwa (Fedha nyingi zimepotea hapo). Kijiji kilitikisika kwa jamko alilolifanya mheshimiwa huyo. Kubwa hapa ni jinsi utamaduni wa Kiafrika usivyoruhusu jambo kama hilo kufanyika/kutokea wala kuzungumzwa.

Kufa ni Lazima: Mwanzo 3:19

Msomaji, hakuna ushindi mkubwa unaozidi kujitayarisha kukabiliana na kifo. Moja ya mambo makubwa mwanadamu anaweza kuonekana alifanya maamuzi magumu na yenye tija, ni kule kujitayarisha ki-usahihi kukabiliana na kifo. Hakuna majuto makubwa kwa mwanadamu yanayoweza kuzidi majuto ya mtu kujikuta hajajitayarisha kukabiliana na kifo.

Nampenda sana Mungu. Yeye hakutuficha katika hili. Aliliweka wazi kabisa kwetu ili kwa mwenye ufahamu aweze kukabiliana nacho. Tutazungumzia vizuri hapo mbele kuhusu kukabiliana na kifo. Lakini Mungu mwenyewe Muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo, aliona umuhimu wa mwanadamu kuelewa kuhusu kufa. Alijua umuhimu wa jambo lenyewe na jinsi mwanadamu anavyotakiwa kujiandaa kukabiliana nacho, yaani asije akakutwa na majuto yasiyo na majibu wala masahihisho.

Biblia Neno la Mungu Linaweka Wazi Kusema

Mungu akimtahadharisha Adamu alimwonya kwamba akikiuka agizo lake na kula matunda ya mti aliomkataza, atakufa (Mwanzo 2:17). Adamu na mkewe (Hawa) wakalifanyia mzaha Neno la Mungu, lakini waliona malipo yake kwa macho yao wenyewe wakati mtoto wao Habili alipokufa. Kwa kuwa hawakuwa wamewahi kuona mtu aliyekufa, lazima iliwachukua muda kuelewa nini kimetokea kwa mtoto wao kwamba hafumbui macho, ahemi wala kutikisika. Ndipo wakakumbuka Mungu alizungumzia neno “Kufa.” Nadhani ndiyo hii!! Wakajikuta wanapasuka kwa kilio kikubwa kisicho kifani wala msaada wowote kwa kuondokewa na mtoto wao mpendwa. Nadhani Mungu aliruhusu jambo hili lisiwaanze wao ili wawe mashuhuda ya matokeo ya madhara waliyoyaleta. Kwa lugha ya mtaani, “Waote joto ya jiwe,” kwa kudharau kwao maonyo na Neno la Mungu. Katika dunia tunayoishi, mwanadamu amejitahidi sana kupambana na kifo, hatukatai wataalamu, wanafanya sehemu yao. Wanatoa vyandarua vya mbu bure ili tusiumwe na mbu wa malaria na tukafa. Wana usemi kwamba wanapunguza idadi ya vifo kutoka asilimia Fulani hadi asilimia Fulani. Wamevumbua madawa na mitambo ya ajabu ya nguvu ya kumpima na kumtibu mwanadamu, hiyo yote ni katika jitihada za kupambana na kifo. Wameweka mpaka vitochi barabarani kuchunguza kasi za magari, hiyo yote ni katika kupambana na kifo. Swala kubwa hapa linalozungumziwa si kupinga jitihada zinazofanywa na wataalamu pamoja na viongozi wetu katika kupambana na kufa. Linalozungumzwa hapa ni kwamba unakubaliana nami kwamba lazima utakufa? Hapa ndipo nataka tusaidiane/umejiweka tayari kukabiliana na kifo? Nalipenda Neno la Mungu lilivyo wazi likimshughulikia mwanadamu kwa kumwambia, “Walio hai wanajua watakufa bali wafu hawajui lolote. Hawana zawadi ingine, hata kumbukumbu juu yao imesahaulika . . . wala hawatakuwa na sehemu yoyote ile kwa yanayoendelea chini ya jua (Mhubiri 9:5). Kifo hakichagui tajiri wala maskini, mtu mashuhuri wala asiye na umashuhuri wowote, mwenye cheo na asiye na wadhfa wowote. Kifo hakina heshima kwa mtu. Ndiyo maana mtu fulani maarufu mwanamume aliyejaa kiburi na kumnyanyasa sana binti mfanyakazi wa nyumbani kwake, wakati wa kukaribia kufa kwake, huku walinzi wakiwa nje na bunduki zao na mke wake akiwa kazini na watoto wake (watu wazima) wakiwa makwao, hali akiwa chooni bila nguo chumbani mwake (master bedroom ya gharama), huku amezidiwa, mauti yanapiga hodi kwa nguvu kumdhulumu roho yake, alilazimika kumwita huyo huyo binti akamwokota humo chooni, akamburuza hadi chini ya kitanda akiwa uchi vilevile bila nguo yoyote ile, na maneno ya mwisho, huku akihema kwa shida alimsimulia binti huyo huyo mbaya wake. Leo Jukwaa linauliza, umejitayarisha kukabiliana na kifo. Mtu anakabiliana na kifo namna gani? Tumwombe Mungu atupe uzima tukutane Jumapili ijayo. Hii ni muhimu sana. Mwambie na rafiki yako na watu wa nyumbani mwako wasome.


BWANA YESU YUKO KAZINI, MAELFU YA WAKAZI WA BURUNDI WAKIINUA MIKONO YAO JUU KAMA ISHARA YA KUMKUBALI KRISTO, KATIKA MKUTANO WA INJILI ULIOFUNGULIWA NA RAIS WA NCHI HIYO PETER NKURUNZINZA. HIVI KARIBUNI

JIFUNZE SHERIA


v Jua haki na wajibu wako kwa mujibu wa sheria

v Jua namna ya kutumia sheria ili upate kufanikiwa.

v Jua ni wapi, lini, kivipi, kwa nani na kwa nini upate haki zako.

v Tambua madhara na hasara za kutojua na kutoitumia sheria ipasavyo.

“NAWE UTAIFAHAMU SHERIA NA SHERIA ITAKULINDA !!!”

SHERIA ZA ARDHI

Karibu katika JUKWAA LA SHERIA. Jukwaa hili litakupa fursa ya kujifunza mambo mbalimbali yahusuyo sheria angalau kwa kiasi fulani, ambayo yatakuwezesha kupata mwangaza mkubwa wa maswala ya sheria. Utafahamu juu ya katiba, haki za binadamu, sheria za jinai, sheria za madai, biashara, mirathi, ndoa, mikataba, usajili na uendeshaji wa makanisa na taasisi nyinginezo na mangine mengi. Katika sehemu hii utajifunza juu ya Sheria za Ardhi. Umekutana na matatizo mengi katika masuala ya ardhi, Jukwaa hili laweza kuwa suluhisho la matatizo yako. Pata maarifa yatakayokusaidia wewe na jamii inayokuzunguka. Karibu !

Katika makala iliyopita tulijifunza juu ya sheria zinazoshughulikia maswala ya ardhi, maana ya ardhi na kanuni za sera ya ardhi na changamoto za ardhi. Naamini zimefanyika msaada mkubwa kwako. Katika makala hii tutaangalia tahadhari unazopaswa kuchukua kabla hujauza, kununua, kutoa au kupokea ardhi pamoja na haki na wajibu ulionao kwa mujibu wa sheria za ardhi. Karibu !

D: Chukua Tahadhari

Upo msemo wa Kiswahili ambao nadhani unaweza kuwa busara kama utautumia ili kukupa muongozo katika kushughulika na maswala ya ardhi. Msemo huu unasema “kinga ni bora kuliko tiba” pia upo mwingine usemao; “chukua tahadhari kabla ya hatari”. Maana halisi ya misemo hii ni kwamba ni bora uchukue hatua za awali za tahadhari kabla ya hatari kutokea. Hatua hizo za tahadhari zitakusaidia sana katika kuondokana au kuepukana na migogoro ya ardhi ambayo umekuwa ukikutana nayo au ambayo unaweza ukakutana nayo. Tahadhari hizo ni kama zifuatazo:-

  • Usinunue shamba, kiwanja au nyumba mpaka ujiridhishe juu ya mamlaka ya muuzaji kama kweli ana mamlaka ya kukuuzia kiwanja hicho.
  • Kama shamba, kiwanja au nyumba hiyo inahusisha mirathi ni muhimu sana anayeuza akawa ndiye msimamizi wa mirathi kwa mujibu wa barua ya usimamizi wa mirathi kutoka mahakamani.
  • Usinunue shamba, kiwanja au nyumba pasipo mkataba halali uliosainiwa kisheria na pande zote mbili na kushuhudiwa na kiongozi wa serikali ya mtaa, kata, hakimu au mwanasheria. (Napendekeza zaidi kwa mwanasheria kuliko sehemu nyingine).
  • Usinunue shamba, kiwanja au nyumba iliyopimwa pasipo kwenda kufanya uchunguzi katika ofisi za ardhi juu ya taarifa sahihi zinazohusu kiwanja hicho.
  • Usinunue au usiuze shamba, kiwanja au nyumba ya familia kwa makubaliano na mume/mke tu bila kupata ridhaa ya mke/mume wake.
  • Usiuziwe kiwanja, shamba au nyumba ambayo hujafika mahali ilipo au hujui mahali ilipo. Hakikisha unauziwa kitu ambacho unakifahamu.
  • Usikubali kupokea kama zawadi shamba, kiwanja au nyumba yoyote kwa maneno tu, pasipo maandishi ya aina yoyote na mashahidi katika makabidhiano hayo. (Napendekeza makabidhiano hayo yafanyike kwa mwanasheria).
  • Usikubali na wala usithubutu kutoa fedha kwa mauziano yoyote ya ardhi pasipo kwanza kukabidhiwa nyaraka za umiliki na mhusika. Pia usikubali kutoa nyaraka zako za umiliki wa ardhi yako pasipo kwanza kupokea malipo halali uliyokubaliana na huyo unayemuuzia eneo hilo.
  • Usinunue shamba, kiwanja au nyumba wala kujenga au kununua nyumba kimya kimya, bila kumshirikisha mume au mke (kwa wanandoa), watoto, ndugu au mtu mwingine yeyote anayehusika katika familia yako. Ukinunua ardhi kisirisiri, utaipoteza kisirisiri.
  • Hakikisha unapata ushauri wa kisheria kutoka kwa mwanasheria juu ya hatua za awali unazopaswa kuchukua kabla ya kununua, kuuza au kufanya matumizi yoyote ya ardhi. Pata pia ushauri kutoka kwa wataalamu wa maswala ya ardhi na mipango miji, viongozi wa serikali ya mtaa, kijiji, kata au wilaya wa eneo hilo ambalo unataka kulinunua kabla hujanunua eneo hilo.

E: Haki na Wajibu Wako Kwa Mujibu wa Sheria za Ardhi

Kumbuka kwamba sheria za ardhi zinaeleza juu ya haki ulizo nazo. Ni wajibu wako kuzifahamu haki hizi ili uweze kujua namna ya jinsi ya kuzipata. Haki na wajibu wako kwa mujibu wa sheria zinaanzia katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho ambayo inakupa haki yako ya kimsingi ya kumiliki mali ambazo ni pamoja na ardhi (ibara ya 24). Haki na wajibu kwa mujibu wa sheria za ardhi zinaweza kuelezwa kama ifuatavyo:-

HAKI

  • Kupatiwa umiliki wa ardhi bila kujali wewe ni mwanamke au mwanaume.
  • Mwanamke kupata, kutumia, kuuza au kutoa ardhi kama ilivyo kwa mwanamume (kifungu cha 3(2).
  • Kupatiwa hati ya umiliki wa ardhi yenye jina, sahihi na picha yako mara baada ya kumilikishwa ardhi.
  • Kuuza, kununua, kutoa au kubadilisha umiliki baada ya kujiridhisha juu ya umiliki halali wa yule anaye kuuzia.
  • Kufungua kesi ya madai ya ardhi yako katika vyombo vya sheria endapo utaona haki yako ya umiliki wa ardhi hiyo inaingiliwa.
  • Kukata rufaa kutoka katika chombo kimoja cha sheria hadi kingine endapo utakuwa hujaridhika na maamuzi yaliyotolewa na chombo husika.
  • Kuweka rehani au dhamana ardhi yako kwa ajili ya kujipatia kipato au shughuli za kibiashara.
  • Kutoingiliwa katika eneo lako unalolimiliki kisheria.
  • Kulipwa fidia stahiki inayoendana na thamani ya ardhi pamoja na mazao au jengo lililopo katika ardhi hiyo endapo eneo lako litachukuliwa na serikali kwa ajili wa matumizi ya umma au shughuli nyingine yoyote ya kiserikali.
  • Kumiliki ardhi kwa pamoja au kibinafsi kati ya mke na mume.
  • Kupata nakala za mikataba au hati yoyote ya umiliki wa yule anayekuuzia, anayekupa au anayekukabidhi ardhi hiyo mara baada ya makabidhiano au mauzo ya eneo hilo.








VIONGOZI WA KITAIFA WA KANISA LA TAG, DR BARNABAS MTOKAMBALI KATIKATI, USWEGE MWAKISYALA WA KWANZA KUSHOTO AKIFUATIWA NA RON SWAI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MKUU WA IDARA YA ELIMU KWA KWANZA KULIA WALIPOKUWA KATIKA SHEREHE FUPI YA KUMUAGA MKURUGENZI WA CHUO CHA AFRIKA MASHARIKI UBUNGO JIJINIDAR ES SALAAM.