OTHER WEBSITE LISTS


Sunday, August 28, 2011

FBI waomba msaada wa kanisa kukamata magaidi



SIKU chache baada ya Ikulu ya Marekani (White House), kutangaza mbinu mpya ya kupambana na magaidi, Shirika la kijasusi nchini humo (FBI), limesema kwamba njia bora ya kuzuia watu hao kutoendelea na michakato yao ni kutumia dini, kutokana na kwamba wao, kwa namna moja au nyingine wanaweza kufanikiwa kwa urahisi tofauti na inavyodhaniwa.

FBI sambamba na mashirika mengine ya Kimarekani yalihimiza hilo wiki iliyopita, ambapo pia waliomba hata wadau hao watakao husika katika zoezi hilo basi wawe wanalipwa papo kwa papo.

Mapema mwezi huu Utawala wa Obama ulitangaza mpango mpya ambao waliugundua katika kuendeleza upingaji wa ugaidi nchini Marekani, ambapo Obama aliwaandikia jumuiya za waislamu walioko nchini humo ambapo watoto wao, familia zao pamoja na majirani zao kuwa ndio wanolengwa katika kuondoa kikundi cha kigaidi cha Al-Qaida na alifanya hivyo kwasababu wanalijua vizuri kundi hilo la kigaidi.

Taarifa ilitahadharisha kuwa wakati katiba ikitangaza uhuru wa kujieleza hata kwa mtu mmoja mmoja kwa habari nzuri au mbaya ni jukumu la serikali kuhakikisha inawashughulikia wale wote wanaokwenda kinyume na kufanya masuala ya kigaidi kwa kuangalia rika jinsia, na kwamba ugaidi wote unaofanywa na watu hao lazima uondoshwe.

“Njia nzuri ya kujilinda na ugaidi pamoja na imani imesha tengenezwa na inaanzia katika familia, jumuia za makundi mbalimbali na katika taasisi,” alisema na kuongeza:

“Umakini wao na uwezo wa kufanya kazi na mtu au taasisi nyingine na hata serikali, ni moja ya kipengele cha historia ya jumuiya yetu, iliyolenga uanzishaji na ushirikishaji wa mpango huu wa wazi kama kuleta changamoto kwa jamii.”

No comments:

Post a Comment