OTHER WEBSITE LISTS


Sunday, June 26, 2011

Atupwa‘jela’ miaka 5kwa kumchapa mwanae

* Jaji aamuru anyang’anywe watoto wote
Texas, Marekani
HUKU akionekana wazi kujawa na hasira kali, Jaji wa Mahakama ya Wilaya katika mji wa Corpus Christi, Texas, Jose Longoria amemhukumu Bi. Rosalina Gonzales, kutumikia ‘jela ya mafunzo maalumu’ kwa kipindi cha miaka mitano na kisha kumnyang’anya watoto wote baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumchapa mwanaye.
Kwa mujibu wa mtandao wa Christians Headlines, Mama huyo aliponzwa na jirani yake aliyemuona mtoto mwenye umri wa miaka miwili akiwa na michirizi ya fimbo mwilini, akashindwa kuvumilia akamnyakua na kumpeleka hospitalini ambapo madaktari walimchunguza na kugundua kuwa alikuwa amecharazwa viboko.
Jirani huyo baada ya baini hilo aliamua kumpeleka mtoto huyo katika kituo cha piolisi ambapo uchunguzi ulifanyika na Bi. Rosalina Gonzales, kutiwa mbaroni kisha kufikishwa mbele ya Jaji ambaye alikuwa mkali mahakamani kama mbogo akilaani hatua ya mtoto huyo kuadhibiwa na mama yake mzazi kwa kuchapwa fimbo.
Mbele ya Jaji majirani walidai kuwa Bi. Gonzales, amekuwa na tabia ya kuwachapa watoto wake wawili ovyo hali ambayo imekuwa ikiwakera mara kwa mara, ndio maana waliamua kufikisha suala hilo mbele ya Polisi ili sheria ichukue mkondo wake.
Jaji Longoria, kabla ya kutoa hukumu kwa mwanamke huyo, alimtolea maneno makali akimuonya kuwa hiyo ni ilani kwake na kwa wanawake wote wenye tabia kama hizo, kwa kile alichodai kuwa nyakati za kuchapa watoto fimbo zimepita.
Kisha Jaji huyo alisema: “Siku hizi hatuchapi watoto, huko nyuma tulikuwa tukifanya hivyo kwa sehemu, lakini jambo hilo lilitufanya tukutane na migongano mbalimbali, usipige tena watoto.”
Sheria iliyotumika kumtia hatiani mama huyo inajulikana kama: “Pretty simple, straightforward spanking case. ”
Sheria hiyo inasema kuwa mtu anayepatikana na hatia ya kuchapa watoto atahukumiwa kuwa katika jela maalumu yenye uangalizi wa mahakama kwa muda wa miaka mitano, huku watoto wake wakiangaliwa katika vituo vya kulelea watoto.
Mama huyo ambaye inaelezwa kwamba si mtu mwenye upendo kwa watoto au mwenye kujua namna ya kulea watoto, mbali na kupewa hukumu hiyo, aliomba kurudishiwa watoto wake, lakini mahakama imesema haitafanya hivyo hadi itakapomuona kwamba amebadilika.
Utamaduni wa kimagharibi unaojali haki za binadamu kupindukia mipaka, ambao unazuia mtoto kuadhibiwa kuwa fimbo umekuwa ukienea kwa kasi katika mataifa yanayoendelea, ambapo mara kadhaa wanaharakati wamekuwa wakiendesha kampeni ya kupinga adhabu ya watoto mashuleni.
Lakini utaratibu huo ni kinyume cha maandiko matakatifu ya Biblia, yanayoonya kuwa mtoto asinyimwe fimbo kwa kuwa itaondoa ujinga.
Andiko hilo linasema: “Ujinga unafichwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.” (Methali 22: 15).

No comments:

Post a Comment