OTHER WEBSITE LISTS


Monday, June 20, 2011

Waraka wa waabudu shetani wasambazwa kwa siri Dar


* Ni maandalizi ya kikao cha Julai nchini
* Wahimizana kufika na damu ya kafara


Na Waandishi Wetu

KILE kinachoelezwa kuwa ni waraka wa siri unaowaalika washiriki wa dini za waabudu shetani  katika mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania, katika kongamano kuu linalotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam, Julai 30, mwaka huu unasambazwa kwa siri kubwa  kama dawa za kulevya, huku ukiambatana na vitisho vikali kwa atakayevujisha siri.
  Gazeti la Jibu la Maisha, limefanikiwa kuunasa waraka huo, unaoonyesha kuwa  umeandaliwa na taasisi inayojulikana kama ‘The Saints Darknes in the world,  Section  (sehemu) ya  WXXX69, ukiwa umeandikwa Mei 23, 2011, ukielekezwa kwa waabudu shetani wa sirini na wale wa wazi wanaoishi na kufanya kazi zao katika mataifa hayo matatu, ambayo ni waanzilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
  Katika aya ya kwanza Waraka huo, unaanza kwa kuwapongeza watendakazi katika ulimwengu wa shetani ukisema:
   “Tunawapa pongezi kwa juhudi zenu juu ya kazi ngumu; tuliyonayo nyakati hizi za mwisho juu ya kuja kwake adui yetu kulichukua kundi lake. Tuna mbinu ambazo kufikia sasa zinaendelea kufaulu na bado zingine zina shida sana upande wetu kuzifanikisha, tungependa kuwaalika rasmi kwenye “kongamano kuu la Afrika Mashariki na kati” mwishoni mwa mwezi 30/07/2011.”
  Kisha unaendelea: “Jambo hili sio la kawaida kwetu,  japokuwa itakuwa mwisho wa mwaka. Lakini mambo yetu yanazidi kuharibika kwa upande wetu na baadhi yetu tukashindwa kutekeleza wajibu wenu, wengine kukosa nguvu kwa kukawia kutoa sadaka zao.”
  Katika maelekezo kuhusu usalama, waraka huo unaagiza: “ Kwa usalama wetu acha tukutane nje ya mji katika lango kuu la kuzimu “Mushitara-Dar es Salaam” saa 6:30 usiku hadi saa 9:00 bila kusahau chupa ya lita 5 za damu na mchanga wa kanisani. Kulingana na lengo letu mambo ambayo tutayazungumzia ni mbinu ambazo tungelifanya ili kuzuia maombi ya adui zetu na kuvunja amani ya jamii kupitia migogoro na migongano ya familia zao hasa kwa viongozi wakuu wa makanisa ya kiroho na kuliwahi kundi lao.”
  Miongoni mwa vipengele tata katika waraka huo uliosainiwa kwa mwandiko unaoashiria lugha ya kiarabu ni kile kinachosomeka: “ Kwa kulifanikisha jambo hili; na watakieni nguvu kupitia kwa alama yetu DWSUD na unasema mara sita; ukiwa umesimama na mara sita umechuchumaa; mara sita ukiwa umelala huku ukiwa uchi (666).”
  Pia waraka huo unatoa amri  kwa wanachama: “ AMRI: Sasa nendeni kwao ili kuharibu nguvu zao kwa kutumia sheria No. 999 WD ili kujificha (usionekane) unapozidi kuwasogelea na kuwafunga wanaume, wanawake na watoto wao. Kumbukeni yule Mwenyekiti wetu wa Afrika Mashariki na kati aliyechukuliwa na adui yetu tangu alipoanza maombi yake mmerudi nyuma sana! Huenda mambo yetu yakawa mabaya zaidi ndio maana tunawahitaji mkapokee nguvu.
  Maeneo hayo tumempa jukumu kupambana naye ni madam- No 1-14-14-18, ambaye kufikia sasa anaendelea kutafuta njia ya kumnasa na kumharibia mipango yake. Hata hivyo kuna mbinu mpya tunayotaka kuwaelezea watu wa eneo hilo. Jaribuni kufanya haraka sana ili kutoa kwa mara nyingine sadaka zenu ili kujiwekea ulinzi.”
  Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa waraka huu hugawanywa kwa watu maalumu tena bila maelezo ya sauti bali hutumia lugha ya ishara.
  Baadhi ya mambo yaliyomo kwenye waraka huo, wenye namba kadhaa za wale wanaelezwa kuwa ni mawakala wa dini za mashetani na waabudu shetani katika ukanda wa Afrika  Mashariki zinazosomeka hivi : “Madam-  No 1-14-14-18.”
  KWA NINI JIBU LA MAISHA LIANDIKE WARAKA HUU TENA NA KUUPA UZITO KATIKA UK. WA KWANZA?
  Baadhi ya mambo yaliyoanishwa katika waraka huu ni yale yanayoonekana makanisani, ambayo yamekuwa yakisababisha migogoro na vurugu kila kukicha. Mfano; miongoni mwa mbinu kuu zinazoelekezwa katika mambo hayo; ni  kwa mawakala hao wa ibilisi kujifanya wameokoka na kujichanganya na makanisa kwa lengo la kuanzisha vita vya ndani.
  Mawakala hawa wanaelekezwa kuhakikisha kuwa wanakuwa na wawakilishi katika kila kanisa lenye idadi kubwa ya waumini au linalokua kwa kasi, na kuhakikisha kuwa wanakuwa marafiki na hata kuhakikisha kuwa wanashiriki kila jambo waaminiwe na baadaye kuanzisha upinzani dhidi ya watumishi wa Mungu.
  Baadhi ya makanisa yanayolengwa  yametajwa katika mfumo ambao huwezi kuyatambua kama si sehemu ya mawakala. Miongoni mwa lugha zilizotumika kuelekeza makanisa ya kushambulia ni hii: “ Jina la kanisa alipo ni M-D-S, na DW-SU: 13-1-3-18-18-9-1.”
  Baadhi ya mikakati inayobainishwa katika waraka huo ni:
1.   Kuzusha magombano baina ya waombezi ili kuwavunja wasiendelee kumtafuta Mungu wao.
2.  Sababisheni hadithi kwa wingi wanapoingia ndani ya makanisa yao wakati wa kuja kumuomba Mungu  wao
3. Msiwaruhusu kuomba wakati wa kulala kwao (janatus) maana hamuwezi kuwaona wakifunikwa na nguvu za Mungu wao
4. Msiwape nafasi ya kusoma Biblia; badala yake wapeni wakati mwingi wa kusoma magazeti; kuangalia televisheni zao.
5.  Sababisheni ufukara; mateso na pesa zao kupotea bila wao kujua ili wasimtolee Mungu wao na walio na pesa roho ya ubahiii ya kutokutoa.
6. Ibada zao ziwe baridi kabisa ili roho wa mungu wao asipate nafasi ya kuongea na kusikia kutoka kwake.
Mwisho waraka huo, unamaliza kwa kuweka namba za msambaza maandishi ambaye anatajwa kama SENIOR URGENT:  KUTOKA MAKAO MAKUU: no. DW-SU: 13-1-3-18-18-9-1
  Ingawa ni vigumu kumpata mwandishi wa waraka huo ili kutoa ufafanuzi, lakini uchunguzi wa Jibu la Maisha, umebaini kuwa karibu mambo yote yanayoelezwa katika waraka huo ndiyo  yanayotokea makanisani na kuwa  kikwazo kikubwa cha kazi ya Mungu.
  Makanisa mengi yamekuwa na migogoro isiyo na sababu ambayo hupoteza muda mwingi katika kuikabili na hata wakati mwingine kuwatoa watakatifu rohoni ili wakajitetee katika hali ya mwili kisheria mahakamani.
 


No comments:

Post a Comment